Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Showing posts with label ELIMU. Show all posts

Tuesday, 13 June 2017

SHEREHE

Ngoma ya Jamii ya kimasai ikitumbuiza katika sherehe ya Mahafali chuo cha Biashara iringa hivi karibuni.

Tuesday, 15 September 2015

NACHANGIA

Mmoja wa wanamafunzo ya uandishi wa habari za Uchaguzi akichangia hoja katika mafunzo yanayo tolewa Kwa baadhi ya wanahabari wa Iringa,Mbeya na Ruvuma katika ukumbi wa Kalenga Hoteli yalio andaliwa na MCT na BBC.

MAFUNZO

Mkufunzi wa waandishi wakujitegemea Atilio Tagalile akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari wa Iringa,Mbeya na Ruvuma juu ya uandishi wa habari za Uchaguzi katika ukumbi wa Kalenga Hoteli Iringa.

UKAGUZI

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akikagua Ujenzi wa Vyoo bora vya wasafiri vinavyojengwa kata ya Mbalamaziwa Wilayani Mufindi Mkoa wa Iringa Barabara itokayo Dar es salaam Mbeya

Friday, 17 July 2015

MUANDISHI WA UHURU NA MZALENDO ACHUKUA FOMU

Dickson Kibiki muandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo akisaini kuchua fomu ya ugombea Ubunge Jimbo la Manispaa Iringa Mjinikama atapata kura za maoni huku mkewe Mrs Tumaini Msowoya akipata kumpiga picha ya kumbukumbu.

Thursday, 16 July 2015

TUNAKUSIKILIZA

Mratibu wa Shirika la TAGRODE  Zuberi Mwachula akiongea na wanakijiji cha Ilalasimba kata ya Nzihi Wilaya ya Iringa katika mkutano wa pamoja na wafadhiri waliofanikisha upimaji aridhi na kupata Hati miliki za kimila kwa kutumia Simu ya Mkononi. sambamba na uelimishwaji sheria ya kumiliki aridhi

940 WAPATIWA HATI MILIKI ZA KIMILA

Frolah Luvanda akipeana mkono na mmoja wa wanakijiji cha Ilala simba baada ya kupokea Hati miliki za Kimila katika khafla fupi iliofanyika hivi karibuni baada ya kufadhiriwa na Umoja wa watu wa Mrekeni CERA kwa ushirikiano na TAGRODE katika mradi wa Mast.upimaji ardhi kwa kutumia simu ya Mkononi.

HATI MILIKI ARIDHI ZA KIMILA

Frolah Luvanda kamishina msaidizi aridhi nyumba na maendeleo ya makazi sehemu ya vijijini akiongea na wana kijiji cha Ilalasimba kata ya Nzihi wailaya ya Iringa baada ya kukabidhiwa Hatimiliki za kimila zilizopatikana kwa upimaji wa kutumia Simu ya Mkononi.Myalu.

Sunday, 26 April 2015

MAFUNZO ELEKEZI BVR IRINGA.

 Neni Guvette akitoa maelekezo kwa maafisa waandishaji matumuzi ya BVR ilinao wakawafundishe waandishaji wasaidizi katika katazao wilayani wanakotoka. Mnyalu.
Maafisa waandikishaji wilaya ya Iringa wakifanyazoezi la upigaji picha kwakutumia Mashine ya BVR wakati wa mafunzo yalioishajana Mkoa wa Iringa. Mnyalu.

MAEUNZO KWA MAAFISA WAANDISHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGAKURA IRINGA SASA.

Afisa muwezeshaji toka Nec taifa Sanif Khalfani akitoa maelekezo ya namna ya Kutumia Mashine ya Kielektronik BVR kwa Maafisa waandikishaji Daftari la wapigakura la kudumu Mkoa wa Iringa. kwa maandalizi ya kuanza rasmi uandikishaji mkoamzima kwa kuanza na baadhi ya vutuo kwa uhaba wa Vifaa vya BVR. Mnyalu.

Thursday, 9 April 2015

UCHAMBUZI WA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015



UCHAMBUZI WA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015

UTANGULIZI

Sheria hii ya Makosa ya Jinai kupitia Mtandao, 2015 ina mapungufu mengi. Mapungufu hayo yamebainika kuwa, kama sheria ikipita yanaweza kuifanya nchi ikawa ni kati nchi adui za matumizi ya mtandao wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano duniani.

Watanzania wote wanatakiwa kufahamu kuwa muswada ukipita utatumika nchini kote yani Tanzania Bara na Visiwani.

Watanzania walio wengi hawafahamu Sheria hii inawahusu kwa namna gani; lakini kwa lugha rahisi ni kuwa itamuathiri mtu yeyote anayeweza tumia Mtandao wa Intaneti kwa kutimia kifaa chochote iwe kompyuta kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama Simu za mikononi, saa, televisheni na vifaa vingine vinavyoendana na hivyo.

Malengo ya Sheria hii ni kuainisha makosa yanayohusiana na matumizi ya mfumo wa kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, kuweka utaratibu wa upelelezi, ukusanyaji na matumizi ya ushahidi wa kielektroniki na masuala mengine yanayohusiana na hayo.

Matumizi ya mitandao yote mikubwa kama Twitter, Instagram, JamiiForums, Facebook, Barua pepe, WhatsApp, blogu na data zote zilizo katika kifaa chochote cha kielektroniki yanaathiriwa kwa kiwango kikubwa na Muswada huu.
UCHAMBUZI

Kifungu cha 7
(1-3): Haibainisha ni aina gani za data ambazo haziruhusiwi kuguswa/kufutwa au zikiguswa/futwa ni kosa la jinai.

7(1g): Kipengele hiki katika kifungu hiki kinarudiwa mara kadhaa katika (Vifungu vya 32-35). Badala ya vifungu vya mbele kurejea kifungu hiki, watunga sheria wameiacha kifungu hiki kikiwa hakieleweki hadi mtu asome vifungu vya mbele.

Je mtu aliyeidhinishwa katika ibara na kipengele hiki ni nani?

Kifungu cha 8:
Muswada huu haujaweka bayana iwapo nyaraka za siri zinaweza kuwekwa wazi katika mtandao kama zina maslahi ya nchi au wananchi mf. Matumizi mabovu ya pesa za umma

Kifungu cha 14:
Neno pornografia halijapewa maana na hivyo jambo lolote lenye mwonekano wa kiasherati (sexually vulgar) linaweza kutafsiriwa kama pornografia na kumuingiza muhusika matatizoni.

Ponografia ya mtandao isikatazwe kabisa ila inatakiwa kuweka ulinzi thabiti wa kuhakikisha watoto hawawezi kufungua mitandao ya aina hiyo.

Ponografia zote ni chafu lakini sio chafu zote ni ponorafia. Hivyo kutokana na kuwa sheria hii inasema ponografia zote ni chafu hii itasababisha kila mtu ahukumiwe chini ya kifungu B.

Uchafu na Ponografia viwe vipengele viwili tofauti.

Kifungu cha 15:
Suala la kujifanya mtu mwingine kwenye mtandao, linaweza kuleta utata kwani kuna baadhi ya mitandao ambapo watumiaji hutumia majina ambayo sio ya kwao. Itakuwaje watu kwa madhumuni mabaya wakitafuta mtu mwenye jina kama hilo na kumshtaki mtumiaji wa mtandao?

Je, mtu kujifanya mtu mwingine inahusisha mtu kutumia jina lisilo lake hata kama hajajifanya mtu mwingine? Ni vema suala hili likafafanuliwa kisheria kwakuwa ni suala muhimu lakini wachache wataelewa manaa yake.

Kifungu cha 16:
Ni nani ana mamlaka ya kubainisha kuwa jambo lililowekwa kwenye mtandao ni la UKWELI, UONGO au UPOTOSHAJI? Ni wazi kuwa mamlaka husika inaweza tumia hili kama mtego kwa manufaa yao.

Kipengele hiki kama vingine kimeambatanisha muda usiopungua bila kusema muda usiozidi. Hivyo mtuhumiwa anaweza kufungwa hata kifungo cha maisha kutokana na mamlaka ya mahakama.

Watu binafsi wanaweza kutumia vibaya kifungu hiki kuzuia uhuru wa maoni kwa kuwaburuza watumiaji wa mtandao mahakamani kila kukicha na kuwapotezea muda wahusika ambao wanaweza kubainika mwishoni kuwa walionewa.

Kifungu cha 20:
Katika mawasililano ya mtandao kama ilivyo mawasiliano mengine kuna ujumbe ambao mtu hawezi kuacha kuupata

Mfano kutembea barabarani na kuona bango la matangazo, au kuwa ndani ya daladala iliyowasha redio.

Vivyo hivyo katika mtandao sio kila ujumbe anaopokea mpokeaji ameuomba na hivyo kifungu hiki kinafanya kila mtu atakayepokea ujumbe bila ridhaa yake kuwa amefanya kosa la jinai.

Kifungu cha 21(1):
Tafsiri za Kiswahili na kiingereza zipo tofauti kabisa.


Tuesday, 2 December 2014

MIAKA 50 YA TAASISI ZA CHUO CHA ELIMU MKWA 28/11/1964- 28/11/2014

Waheshimiwa wakikata utepe kuzindua machapisho ya Chuo kikuu cha elimu kishiriki  (MUSE)
  Picha na Mnyalu

Saturday, 24 May 2014

WASHIRIKI SEMINA YA PSPF RUCO IRINGA

Wanafunzi wa Mwaka wa Mwisho Chuo kikuu cha Ruaha Iringa wakipatiwa semina juu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa uma Tanzania PSPF.
Mnyalu

AFISA MFAWIDHI MFUKO WA PENSHENI KWA WATUMISHI WA SERIKALI.

Wanafunzi wa Chuo kikuu Ruaha Iringa wakimsikiliza Baraka Jumanne Afisa Mfawidhi mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa serikali Iringa namna mfuko huo unavyo fanya kazi kwa watejawake.
Mnyalu

MAAFISA PSPF WATOA ELIMU YA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII WATUMISHI WA SERIKALI RUCO.

Wanachuo cha RUCO wakimsikiliza Afisa wa PSPF Iringa akitoa maelezo ya Mfuko wa hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa serikali Tanzania na namna ya kujiunga.
Mnyalu.

Thursday, 15 May 2014

SHULE ZA SEKONDARI ZILIZO FANYA VIZURI KITAIFA MUFINDI ZA ZAWADIWA.

Mkuu wa Wilaya Mufindi Evarista kalalu akimkabidhi Sr Jeslin Sabs  Cheti cha Ufauru pamoja na Ngao  kwa ajili ya Shule ya Sekondari ya Wasichana Bethel Sabs  Mafinga kwa kushika nafasi ya 7 kitaifa kwa ufauru ikiwa na Idadi ya wanafunzi chini ya Arobaini  hafra hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Halmashauri Mufindi chini ya Wizara ya Elimu na mafunzo ua ufundi.Tanzania. Mnyalu.

Wednesday, 14 May 2014

MB MUFINDI KASKAZINI ATOA VIFAA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI.


Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista kalalu akikabidhi  Kompyuta mbili  Paulo Mahimbi  Mw /Mkuu shule ya Msingi Ugesa moja kati ya Kompyuta 5 zilizo tolewa na Mh Mahammod Mgimwa. Mnyalu.
Iringa.Halimashauri ya wilaya ya mufindi inakabiliwa na 
upungufu wa madawati 4269 kwa uwiano wa dawati moja kwa wanafunzi wawili wakati awali wilaya hiyo ilikuwa ikisifika kwa utumiaji wa madawati ya Adobe licha ya  wilaya hiyo kuvuna mbao.
Hayo yalibainishwa juzi wakati wakipokea madawati  100 na kompyuta 5 zenye thamani ya shilingi mil 12 kutoka kwa Naibu waziri wa maliasili na utalii Mh Mohamud Mgimwa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la mufindi kasikazini kwa kushirikiana na mfuko wa penseni kwa watumishi wa uma(PSPF) Iringa.
 Mgeni rasimi katika makabidhiano hayo mkuu wa wilaya ya mufindi Evarista Kalalu alisema kuwa wilaya ya Mufindi haina upungufu wa madawati kwa uwiano wa dawati moja kwa wanafunzi wawili upungufu uliopo niwa walimu wa sayansi kitendo kinacho sababisha kutokuanya vizuri katika somo hilo.
“Wakuu wa shule kwa kuwa mufindi haina upungufu wa madawati upungufu uliopo ni wa walimu wa sayansi hivyo nawaombeni masomo yaliyosalia yaweze kuleta matokeo mazuri shuleni”alisema Kalalu
Kwa upande wake Afisa elimu msingi Mufindi Farida Mwasumilwe alisema kuwa wanashukuru kupokea vifaa hivyo kwa sababu wanahitaji kuboresha ili uwiano uwe kwa dawati moja kwa mwanafunzi mmoja ili waweze kujitegemea katika mtihani wa mwisho.
“Nawashukuru wadau mbali mbali ambao wanajitokeza katika kuweka nguvu katika sekta ya elimu na madawati haya yanaenda katika shule ya msingi mjimwema,Mamba,  nyamalala na  kompyuta zinaenda shule za msingi  Ugesa, Itona na Igombavanu sekondali.”alisema Farida
Naye Baraka Jumanne Ofisa mfawidhi mkuu wa  PSPF Iringa aliwataka walimu hao pamoja na wanafunzi kuvitunza vifaa hivyo ili vidumu na vitumike kwa wanafunzi wengine wanaotarajiwa kuanza masomo.
Mnyalu.

MWISHO.

Tuesday, 13 May 2014

MBUNGE MUFINDI KASKAZINI ATOA VIFAA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI MUFINDI KASKAZINI

Afisa Elimu  Msingi wilaya ya Mufindi Farida Mwasumilwe akiongea kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Mufindi Evarista Kalalu wakati wa Hafla fupi ya kukabidhi Kampyuta tano na Madawati miamoja kwa Shule za Msingi na Sekondari Vifaa hivyo vimetolewa na Mbunge wa Mufindi Kaskazini Mahammodu Mgimwa Pamoja na Shirika la Mfuko wa Pensheni wa watumishi wa Uma  Mkoa wa Iringa..Mnyalu.

AFISA PSPF IRINGA AKIONGEA NA BAADHI YA WAALIMU MUFINDI KASKAZI

A
Afisa Mfawidhi  Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Serikali  Mkoa wa Iringa Baraka Jumanne akiongea na waalimu wa Shule za Msingi tatu Mufindi kaskazini  pamoja na maafisa Elimu walio hudhuria kabla ya kukabidhi madawati Mnyalu.

Saturday, 3 May 2014

Daftari la wapiga kura kuboreshwa



Watu zaidi ya 2,500 wanahofiwa kufariki dunia baada ya kufukiwa na mmomonyoko wa ardhi Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo katika Jimbo la Badakhshan..Mwananchi,..