Mwamuzi wa mpira wa Lipuli sc na Kimondo Fc Krina Kabara akitolewa nje kukwepa ugonvi uliokuwa unaendelea uwanjani hapo baada ya mpira kumalizika...
Iringa.
MWAMUZI wa mpira
kati ya Lipuli Sc ya mjini Iringa na Kimondo Fc ya Mbalizi Mbeya Krina Kabara uliochezwa jana katika
kiwanja cha Samora na kutoka sare ya goli moja anusulika kupigwa kwa madai ya
kupendelea timu moja na kuisababishia Lipuli isipande daraja.
Mashindano
hayo ya ligi daraja la kwanza ambayo
yanaendelea yalisababisha muamuzi huyo kushambuliwa kitendo kilicho sababisha
mashabiki pamoja na baadhi ya wachezaji kumshutumu mwamuzi huyo kuwa amechezesha mchezo huo kwa
matakwa ya mwenyekiti wa Lipuli.
Lipuli
sc ilijipatia goli la kwanza kunako dakika ya 3 ambalo lilifungwa na Abdala
Matimila katika kipindi cha kwanza na BarakaMtafya wa Kimondo Fc aliifungia timu yake kwa penati kusawazisha goli hilo dakika ya 9 .
Akizungumza
mwenyekiti wa Lipuli Sc Abuu Chang’aa alisema kuwa tuhuma za kuwa kauza mechi
kwa kuwapa wachezaji wa Lipuli fedha ili
wacheze chini yakiwango si kweli
kwasababu anapenda maendeleo ya timu hiyo na anataka izidi kusonga mbele zaidi.
“Mimi
siwezi kuwalipa wachezaji ili wacheze chini ya kiwango pesa nilizo wapa ni kwa
ajiri ya usajiri wengine hawakuwa wamemaliziwa kulipwa,kama hawawezi na hawana
imani na timu yao waache kuchezea”alisema Abuu
Abuu
aliongeza kuwa mechi ijayo Lipuli inatarajia kucheza na timu ya Majimaji Fc na
Mlale ya mjini songea ambapo wataondoka alihamis wiki hii kuelekea Songea kwamichezo hiyo ambapo Lipuli inapointi 14 na kimondo inapointi 11.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment