Sunday 27 April 2014

Umuhimu wa kula mboga mbichi





Ulaji wa mboga mboga zikiwa katika hali ya ubichi au zikiwa hazijapikwa una faida kubwa kiafya. Hata hivyo, ulaji huo bila ya kuchukua tahadhari utasababisha magonjwa yanayoenea kutokana na kula vyakula vichafu.

Katika maisha ya binadamu karibu kila jambo zuri linatakiwa kufanywa kwa tahadhari au kuchunga miko yake. Bila ya kufanya hivyo, faida ya jambo hilo haitapatikana na badala yake maafa yatachukua nafasi.
Ulaji wa mboga mboga zikiwa katika hali ya ubichi au zikiwa hazijapikwa una faida kubwa kiafya. Hata hivyo, ulaji huo bila ya kuchukua tahadhari utasababisha magonjwa yanayoenea kutokana na kula vyakula vichafu.
Moto unaharibu
Ni ukweli wa miaka mingi kuwa kupika au kutumia moto katika kuandaa vyakula kuna haribu virutubisho vinavyopatikana katika mboga mboga.
Mboga za majani ambazo hazijakomaa na mbichi ni chanzo kikubwa cha vitamini na madini ya aina mbalimbali. Mboga hizo endapo zitakamuliwa na kutumiwa kama juisi, faida yake kiafya itakuwa kubwa hasa kwa wagonjwa.
Mboga mboga zinaondoa tindikali inayozalishwa wakati vyakula vingine vikisagwa tumboni kama vile nyama na jibini.
Mboga za majani za kijani ni chanzo kikubwa cha carotene ambayo inabadilishwa mwilini na kuwa vitamini A.
Mboga mboga pia, ni chanzo kizuri cha vitamini C.
Vitamini A ina kazi kubwa ya kuimarisha macho ili yaone vizuri hasa wakati wa giza.
Inasaidia pia ukuwaji na ufanyaji kazi wa chembehai na kuimarisha kinga ya mwili.
Vitamini C ina kazi nyingi ikiwemo kuimarisha ufanyaji kazi wa chembehai, inaimarisha kinga, kuponya mafua na vidonda.
Baadhi ya mboga mboga zina protini na wanga. Kwa mfano, maharage na kunde ni chanzo kikubwa cha madini ya chuma na protini. Viazi mviringo na viazi vitamu ni chanzo kikuwa cha wanga.
Mwananchi

 

Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment