Showing posts with label MATUKIO. Show all posts
Showing posts with label MATUKIO. Show all posts

Tuesday, 2 June 2015

MAONYESHO YA UTENGENEZAJI VITAMBULISHO VYA KITAIFA.

Washiriki toka Mataifa mbalimbali wakiangalia mashine za uandaaji vitambulisho vya kielekroniki wakati wa Mkutano wa kwanza Afrika ulioanzaleo katika ukumbi wa Serena Hoteli ukiambatana na maonyenyo ya ainambalimbali za Mashine Dar es salaam Mnyalu

AJARI YA ZUA FOLENI KUBWA BUGURUNI LEO

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wakitafuta njia mbadala baada ya ajari ya Treni iliogongwa an Gari aina ya Scania T507AVW.mali ya Bw Mohamoud Mohamed wa Duale Traspotrt Ltd wa Dar es salaam. Mnyalu.

Thursday, 2 April 2015

KERO .MTAANI. IRINGA

Vijanawakiokota vitu chakavu jalalaniManispaa Iringa

Wednesday, 19 February 2014

AJALI LEO ASUBUHI ENEO LA TANESCO IRINGA,

 
 Gari No,T156 BJR na T300BGM zimegongana katika  Barabara kuu Iringa Mjini hakuna madhara yeyote.

Saturday, 15 February 2014

Rais Kikwete: Kuna majangili papa 40 nchini


Habari Kuu

Posted 5 hours ago
>Wakati kuna joto la vyombo vya habari vya kimataifa kuituhumu Tanzania kuwa haipambani na ujangili, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali imeubaini mtandao unaojumuisha watu 40, akiwemo tajiri maarufu mkoani Arusha....
Chanzo Mwananchi
Mnyalu.

Yanga yatisha, Komorozine wakubali kufa

 

Wachezaji wa Yanga wakijianda kwa mazoezi kwenye Uwanja wa Mitsamiouli mjini Moroni, Comoro
Chanzo mwanaspot.. 

Thursday, 13 February 2014

Amuua mwenzake wakigombea sigara

images_19a23.jpg
Tanga. Uvutaji wa sigara umeleta maafa, baada ya mtu mmoja kukatwa mkono na kuuawa na mwenzake wakati wakigombea sigara.
Katika tukio hilo lililotokea Korogwe, Jumapili iliyopita, Februari 2, mnamo saa nne asubuhi, Idi Mkono, mwenye umri wa miaka 30 alimkata mkono Ramadhani Gudelo (35) na kumuua baada ya kutokea ugomvi uliohusu sigara.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Constantine Massawe alisema kuwa Polisi Tanga wako katika msako mkali wa kumtia nguvuni Iddi Mkono (30) kwa tuhuma za mauaji.
Kamanda Massawe ameitaka jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi, badala yake wafuate taratibu na sheria zilizopo.
Wakati huo huo, watu wawili wanashikiliwa na polisi, mkoani hapa kwa tuhuma za kukamatwa na lita 147 za pombe haramu ya gongo maeneo ya Handeni, mkoani Tanga.
Kamanda Massawe alisema kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa watuhumiwa hao lilitokea Februari 2 mwaka huu saa 5:30 asubuhi.
Massawe aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Hussen Muhadu (48), pamoja na Ramadhani Ugarawe (40), wote wakazi wa Chanika Handeni.
Alisema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayowakabili.
Aidha Kamanda Massawe aliwaonya wananchi kuchukua tahadhari na matendo ya uhalifu wa aina yoyote ambao unaweza kusababisha kuvunja sheria, huku akionya kuwa kwa yeyote atakayekiuka sheria zilizowekwa atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.
CHANZO:MWANANCHI

KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI YAANZA KUSIKILIZWA

Na: BerdinaMajinge,Iringa

MAHAKAMA kuu kanda ya Iringa imeanza kusikiliza kesi ya muuaji wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha channel ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi huku vituko na visa baina ya wanahabari na askari wa jeshi la polisi mkoani Iringa vikiendelea kuchukua sura mpya hali inaleta maswali miongoni mwa wafuatiliaji wa kesi hiyo.
katika kesi hiyo wakili wa serikali Adolph Maganda amedai mahakamani hapo mbele ya Jaji Mary Shangali kuwa mnamo tarehe 2 septemba mwaka 2012 askari no g. 2573 wa jeshi la polisi kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Iringa Pasificus Ceophace simon alimuua Daudi Mwangosi kwakukusudia kinyume na kifungu cha kanuni ya adhabu no 196 sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002
Wakili huyo wa serikali amewasilisha mahakamani hapo vielelezo vya ushahidi wa kesi hiyo ikiwemo ripoti ya kitabibu iliyotolewa na mganga aliyefanyia uchunguzi mwili wa marehemu mwangosi, kitabu cha kumbukumbu za kutoa na kurudisha silaha kituoni, ripoti ya mtaalam wa milipuko, mahojiano ya ungamo na onyo pamoja na gazeti la mwananchi la tarehe 3 septemba 2012 lenye picha ya mtuhumiwa akiwa ameshikilia silaha aliyoitumia kumfyatulia marehemu
Hata hivyo mtuhumiwa licha ya kukiri kuwepo katika eneo la nyololo wilayani mufindi siku hiyo ya tukio amekana shitaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa mpaka hapo itakapopangiwa siku ya kusikilizwa tena na mtuhumiwa amerudishwa rumande
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mwandishi wa habari wa magazeti ya Dairy News na Habari leo mkoani iringa Frank Leonard alikamatwa na polisi kwa tuhuma za kupiga picha wakati mahakama ikiendelea ambapo alishikiliwa kwamuda na baadae kufikishwa katika kituo cha polisi iringa kabla ya kuachiwa bila kuandika maelezo.
mwisho

MWENYEKITI IRINGA PRESS CLUB AKAMATWA NA KUACHIWA

Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Iringa 
 Frenck Leonard akiongea na waandishi baada ya kuachiwa na Polisi  alipo kamatwa ndani ya mahakama wakimtuhumu kuvunjasheria wakati akisikiliza kesi ya Mshitakiwa wa mauaji ya Daud Mwangosi aliekuwa mwandishi wa Chanel ten na Mwenyekiti wa (IPC)
 Waandishi wa habari Wakiwa viwanja vya mahakama ya wilaya iringa wakisubili kupata maelezo kwa msajili wa mahakama juu ya kitendo cha Polisi kumkamata Mwennyekiti  wa IPC wakimshuku kuvunja sheria ndani ya mahakama kosa ambalo halikujulikana nakupeleke kumuachia huru.
Askari kanzu wakimpa ulinzi mtakatifu mshitakiwa wa kosa la mauaji ya aliekuwa muandishi wa chanel ten Daudi Mwangosi wakati ana toka mahakamani leo kwa kumpandisha katika gari maalumu ili asipigwe picha na waandishi baada ya kesi yake kuandikishwa rasimi katika mahakama kuu na itajadililiwa katika kikao kitakacho pangwa tayali kwa kusikilizwa
Mnyalu.

Wednesday, 8 January 2014

AJABU NA KWELI YA MWAKA 2014.


Uyoga
Picha na Mnyalu

UZINDUZI WA MICHEZO NA ELIMU YA STADI ZA MAISHA KATA YA IKWEHA MUFINDI KASKAZINI


 Mh Mahammoudu Mgimwa akimkabidhi nahodha wa timu ya kijiji cha Ikweha Baraka Ruhanzo
Mpila kwa ajili ya mazoezi kujiandaa na mashindano.
 Mh Mahammoudu Mgimwa akizindua mashindano ya Mgimwa Cup kwa kupiga Danadana
 kabla ya Mchezo.
Timu zilizo fungua mashindano zikisalimia mashabiki waliofika kabla ya Mpambano.
Picha na Mnyalu.


  Mashindano ya mpira wamiguu yamezinduliwa Tar 01/01/2014 na Mh Mahamudu Mgimwa Mbunge wa jimbo la Mufindi kusini katika Tarafa ya sadani kata ya Ikweha  kijiji cha Ugenza.
Mashindano hayo yameanzishwa na kusimamiwa na shirika la Mgimwa foundation pamoja na umoja wawanafunzi walio maliza vyuovikuu wilayani mufindi (MUYOWIRUDE)
Akiohutubia wananchi wa kata ya Ikweha pamoja na wanamichezo waliohudhuria katika kiwanja cha Shule yamsingi katanihapo kabla ya uzinduzi.
 Mh Mgimwa alisema nidhamira yake na viongozi anaoshirikiana nao kuhakikisha vijana katika jimbo lake wananufaika kwa kupitia michezo nahasa kwa msimu huu kaanza na kata ya Ikweha
Mashindano hayo yatajumuisha timu tano za kata hiyo nazo ni kutoka katika vijiji vya Ikweha,Ugenza,Ilangamoto, Sinai pamoja na Ukeremi.
Akizungumzia zawadi Mh mgimwa alisema Mshindi wa kwa nza atapata jumla ya Track suti 16 zenye thamani ya shiringi 480,000/=pamoja na mipira miwili yenye thamani ya shilingi 150,000/= jumla yake ni Tshs. 630,000/=
Mshindi wa pili atazawadiwa seti ya Jezi yenye thamani ya shilingi 150,000/=pamoja na mipira miwili ya Shilingi 150,000/= jumla yake ni Shilingi 300,000/=
Mshindi wa tatu atapata mipira miwili yenye thamani ya shilingi 150,000/= awali Mh mbunge Mahamodu Mgimwa alitoa seti ya Jezi katika kila timu pamo na mpira mmoja wa mazoezi.
Pia alikabidhi mipira miwili kwa waamuzi wa mashindanohayo kwaajili ya kushindania sambamba na hilo Mh mgimwa atatoa zawadi zifuatazo.
  Mfungaji wa goli la kwanza katika mashindano hayo atapata shilingi 20,000/=,Mchezaji mwenye nidhamu atapata shilingi 30,000/= pia timu yenyenidhamu itapata shilingi 50,000/= na Mchezaji bora atapata shilingi 50,000/=
Akiwaasa vijana kwa kupitia mashindano hayo Mh Mgimwa alisema vijana wawewasikivi watakapo kuwa wakipatiwa mafunzo ya stadi za maisha kwakupitia wawezeshaji toka shirika la (MUYOWIRUDE).
Ambao wataenda sambamba na michezo hiyo kwani watapa kujifunza bure aliwaomba wajitokeze kwa wingi.
Nae Marko Shayo kiongozi wa NG’OS (MUYOWIRUDE) alisema wao watatoa elimu yanamna yakujikinga na maambukizi ya Ukimwi,Elimu ya Ujasiriamali kwakutumia
Rasilimali zinazo wazunguka katika mazingira yao hukohuko vijijini pia elimu ya jinsia na unyanyapaa katika jamii.
Akizungumza na mwandishi Nd,Albrto Chaula mkazi wa kata ya Ikweha alisema wamepokea kwafuraha mashindano hayo yatakayoenda sambamba na upataji waelimu ya stadi za maisha kwani waosasa jukumulao ni kujitokeza kwa wingi iliwapate faida itakayo wafaa maishani.
Mwisho.
Said Ngamilo.        

SALAMU YA HERI YA MWAKA MPYA.



 Mh. Mchungaji Peter Msigwa mbunge wa Iringa mjini akiwahutubia wananchi wa Manispaa ya Iringa 
Tar 31/12/2013 katika viwanja vya mwembetogwa kuwatakia heri ya mwaka mpya
Pamoja na mustakabari wa hali ya kisiasa na utendaji wa serikali nchini.
Mnyalu.






STADI ZA MAISHA YA JAMII YETU.


Stadi za kazi kwa watoto waishio vijijini huwa ni kwa vitendo zaidi  picha hizi kijijini Mtitu kata ya Mtitu Wilaya ya Kilolo.
  Kilimo kwanza ni dhana inayosemekana na kufikirika ila haijatendeka ipasavyo vijijini.
 
 Wanyama kazi na changamoto zake wakati wa matumizi vijijini hapa ni kijiji cha Kitowo kata ya Mtitu Wilaya ya Kilolo.
.
Usafiri wetu.
(Picha zote na Mnyalu)

Tuesday, 7 January 2014

JIWE LA MSINGI


 
Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho kikwete akiweka jiwe la msingi katika Barabara ya Iringa – Dodama katika eneo la kijiji cha Migori wilaya ya Iringa mwaka jana.
Picha na Mnyalu.  


MJI WA IRINGA



Mji wa Iringa eneo la stendi kuu unavyoonekana katika picha.
Picha na Mnyalu.

MSAADA WA VIFAA HOSPITALI






Meneja wa Radio Nuru Victor Chakudika   akikabidhi  msaada wa vifaa vya kutembelea wagonjwa kwa Muuguzi Mfawidhi Rustika Tung’ombe katika haspitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa katika kusherehekea heri ya mwaka mpya.
Picha na Mnyalu.