Wednesday 14 May 2014

MB MUFINDI KASKAZINI ATOA VIFAA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI.



Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista kalalu akikabidhi  Kompyuta mbili  Paulo Mahimbi  Mw /Mkuu shule ya Msingi Ugesa moja kati ya Kompyuta 5 zilizo tolewa na Mh Mahammod Mgimwa. Mnyalu.
Iringa.Halimashauri ya wilaya ya mufindi inakabiliwa na 
upungufu wa madawati 4269 kwa uwiano wa dawati moja kwa wanafunzi wawili wakati awali wilaya hiyo ilikuwa ikisifika kwa utumiaji wa madawati ya Adobe licha ya  wilaya hiyo kuvuna mbao.
Hayo yalibainishwa juzi wakati wakipokea madawati  100 na kompyuta 5 zenye thamani ya shilingi mil 12 kutoka kwa Naibu waziri wa maliasili na utalii Mh Mohamud Mgimwa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la mufindi kasikazini kwa kushirikiana na mfuko wa penseni kwa watumishi wa uma(PSPF) Iringa.
 Mgeni rasimi katika makabidhiano hayo mkuu wa wilaya ya mufindi Evarista Kalalu alisema kuwa wilaya ya Mufindi haina upungufu wa madawati kwa uwiano wa dawati moja kwa wanafunzi wawili upungufu uliopo niwa walimu wa sayansi kitendo kinacho sababisha kutokuanya vizuri katika somo hilo.
“Wakuu wa shule kwa kuwa mufindi haina upungufu wa madawati upungufu uliopo ni wa walimu wa sayansi hivyo nawaombeni masomo yaliyosalia yaweze kuleta matokeo mazuri shuleni”alisema Kalalu
Kwa upande wake Afisa elimu msingi Mufindi Farida Mwasumilwe alisema kuwa wanashukuru kupokea vifaa hivyo kwa sababu wanahitaji kuboresha ili uwiano uwe kwa dawati moja kwa mwanafunzi mmoja ili waweze kujitegemea katika mtihani wa mwisho.
“Nawashukuru wadau mbali mbali ambao wanajitokeza katika kuweka nguvu katika sekta ya elimu na madawati haya yanaenda katika shule ya msingi mjimwema,Mamba,  nyamalala na  kompyuta zinaenda shule za msingi  Ugesa, Itona na Igombavanu sekondali.”alisema Farida
Naye Baraka Jumanne Ofisa mfawidhi mkuu wa  PSPF Iringa aliwataka walimu hao pamoja na wanafunzi kuvitunza vifaa hivyo ili vidumu na vitumike kwa wanafunzi wengine wanaotarajiwa kuanza masomo.
Mnyalu.

MWISHO.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment