Tuesday 30 December 2014

WAMILIKI SIRAHA KINYUME CHA SHERIA KUKIONA



WANAO MILIKI SIRAHA KINYUME CHA SHERIA  WATAKIWA KUZISALIMISHA HARAKA.
Mkuu wa wilaya Iringa  Dr Leticia  Warioba awataka wananchi wa Halmashauri ya Iringa wanao miliki siraha kinyume cha sheria kuzisalimisha haraka iwezekanavyo kuanzia Tar 30-12-2014 mpaka tar 01-02-2015 bila shuruti yeyote atakae fanikisha zoezi hilo hatachukuliwa hatuazozote dhidi yake.
Akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake majira ya Saa nane Mchana Dr Leticia Warioba alisema anawaomba wananchi watoe ushirikiano kufanikishahilo kwani yeye na kamatiyake ya Ulinzi Kiwilaya wameazimia kuhakikisha wanapambana vilivyo  na mautukio ya Uvunjifu wa amani na Ujangili wa Tembo katika Hifadhi za Ruaha.
Akifafanua zaidi alisema Siraha zisalimishwe katika Ofisi za watendaji Miji/viijiji au ofisi za watendaji kata na Vituo vya Polisi vilivyo jirani na wananchi. Sambamba na hilo aliwataka viongozi wahusika kutoa ushirikiano wa dhati katika zoezihilo huku akibainisha kuwa baada ya tarehe 1-02-2015 kupita Msakomkari utapita Nyumba kwa Nyumba na atakae bainika kukutwa na Siraha hatua kari dhidi yake zitachukuliwa kwa kufikishwa katika vyombo vya Sheria.
Pia aliwatakia wananchi wa Wilaya ya Iringa na Vitongoji vyake Heri ya Mwaka Mpya na kusherehekea kwa amani na utulivu ilikuingia mwaka mpya wa 2015 kwa utulivu  huku akikumbusha dhana ya ulinzi shirikishi iendelee kufanyakazi  katika jamii ili kudumisha amani.
Said Ng’amilo  Iringa.

Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment