Mh Jesca
Msambatavangu Mwenyekiti wa CCM Mkoa Iringa akiongea na waandishi wa
Habari katika Ofisi ya IPC Iringa leo kujibu tuhuma dhidi yake toka
katika kamati ya Maadili ya Wilaya CCM Manispaa ya Iringa akiazimia
kukata Rufaa hivikaribuni.
Picha na
Said Ng'amilo.
PRESS RELEASE- SITOFAHAMU ILIYOJITOKEZA BAADA YA MAAMUZI
MBALI MBALI KUFANYIKA NA KUTANGAZWA KUHUSU MAADILI YA UONGOZI.
UTANGULIZI
Mtakumbuka kuwa tarehe 2/3/2015 kuna
kauli ambayo ilitolewa na Katibu wa wilaya ya Mufindi Ndugu Mtaturu. Ambayo ilielekeza
baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Chama cha Mapinduzi kwa baadhi ya wanachama
wetu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa uanachama kwa baadhi ya makada wetu. Akiwemo
Shukuru Luhambati, Clara Shirima na Hosea Kaberege. Swala hili limeamusha
malalamiko na mjadala miongoni mwa wanaCCM na wapenzi na wakereketwa wa CCM.
Kila mtu akiwa na mtizamo wake kuhusu swala hili, ambalo pia kimepelekea
kuamsha malumbano katika vyombo mbali mbali vya habari.
Lakini pia kumetokea wasi wasi mkubwa
kwa baadhi ya wanachama ambao walihojiwa na kamati za maadili na kuwa na uvumi
pia kuwa watafukuzwa au kunyang’anywa uanachama.
Hiyo pia imeleta uvumi kuwa Mimi
Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa pia nimesimamishwa uanachama na kuvuliwa
nafasi zote za uongozi.
Moja, Sitofahamu iliyojitokeza kwa wale walioachishwa UANACHAMA: (Shukuru
Luhambati, Clara Shirima na Hosea Kaberege)
Kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM. Toleo la 2010
zilizotolewa na Halshauri Kuu ya Taifa. Fungu la Nne (8vi) pg 30 linalohusu
adhabu mbali mbali kwa makosa yanayohusu ukiukwaji wa Maadili. Inasema katika
kipengele hicho:
(vi) Kuachishwa Uanachama:
MwanaChama anayegundulika ana makosa ya Itikadi, yanayoathiri Uhai wa
Chama, au ambaye ameshindwa huko nyuma kujirekebisha hata baada ya Karipio,
wala haonyeshi dalili za kuweza kujirekebisha hata akipewa muda zaidi, basi
Kamati ya Usalama na Maadili ya Taifa inaweza kupendekeza mbele ya Kamati Kuu
mwanachama huyo aachishwe UANACHAMA. Ikiridhika, Kamati Kuu itapeleka shauri
hilo mbele ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa uamuzi wa mwisho.
(a)Adhabu ya kuachishwa Uanachama itatangazwa hadharani.
Pia Fungu la Tatu linalohusu: WAJIBU WA KUSIMAMIA TABIA, MWENENDO NA VITENDO VYA MWANACHAMA NA
KIONGOZI;
Ni wa vikao vya Chama cha Mapinduzi
vya Halmashauri kuu na Kamati zake za Siasa kwa kila ngazi kama ilivyoanishwa
kikatiba.
Kwa swala la leo hapa: Ibara ya 93(8), (14) na (15), Halmashauri
Kuu ya CCM Mkoa:-…….(14) Kumwachisha au kumfukuza Uanachama Mwanachama ye yote
endapo itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za
uanachama. Mwanachama anayeachishwa au
kufukuzwa uanachama anaweza kukata rufaa kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya
Taifa.
Hivyo basi, hakuna
sababu yakuwa na hofu au mashaka. Wale ambao wanadhani hawajatendewa haki
wanahaki ya kukataa rufaa vikao vya juu zaidi, kama Kamati Kuu ya Halmashauri
Kuu ya Taifa.
Pili, Kuhusu Mwenyekiti wa CCM Mkoa
kusimamishwa Uongozi sio kweli. Ibara 93 (15) fungu la tatu. Halmashauri Kuu ya
Mkoa; Inaweza Kumwachisha au Kumfukuza Uongozi kiongozi ye yote ambaye uteuzi
wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa.
Pia,Ibara 95(7) Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa;
Kumsimamisha uongozi kiongozi ye yote wa ngazi ya wilaya endapo
itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uongozi.
Isipokuwa kwamba haitakuwa na uwezo wa kumsimamisha uongozi kiongozi ambaye
uteuzi wake wa mwisho haukufanywa na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.
Kwa nafasi yangu mimi kama Mwenyekiti
wa Mkoa siwezi kusimamishwa uongozi na ngazi ya Mkoa. Hata pia kwa nafasi ya
Diwani lazima ipelekwe vikao vya ngazi ya Taifa.
Ingawa wilaya ya Iringa Mjini kupitia
Katibu wake Zongo Lobe Zongo wamenipa Adhabu mimi Mwenyekiti wa Mkoa kwa Kupewa
Adhabu ya Onyo Kali. Taratibu nyingine zitafuatwa kwa mujibu wa vikao.
Nina toa maelekezo pia kwa Kamati za
Maadili zote katika ngazi zote za Mkoa wa Iringa kuzingatia kanuni, Katiba na
maelekezo ya Chama katika utekelezaji wao wa Kazi zao za Kamati ili
kutoviyumbisha vikao vya maauzi vya Chama. Pia ili kuondoa mgongano unaweza
ukajitokeza kati ya viongozi, wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi kwa
ujumla wake. Kwa mujibu wa Kanuni za uongozi na maadili toleo la 2012; fungu la nne
7(1)…”Katika kusimamia maadili ya viongozi wa CCM wakati wo wote wa utekelezaji
wa kanuni hizi, ..Kamati ya Usalama na maadili katika ngazi inayohusika
(mkoa) itazingatia Katiba ya CCM na
Kanuni zingine za CCM zitakazo kuwepo wakati huo, pamoja na maelekezo mengine
ya msingi yatakayokuwa yametolewa na Halmashauri Kuu ya Taifa”.
Ninawasisitiza kuzingatia zaidi;
Kanuni za Uongozi na Maadili fungu la
Nne 7(4)ii-kinachohusu Tuhuma: Kinasema
”Uchambuzi wa tuhuma hizo utafanywa kwa kutumia njia mbali mbali pamoja
na mashahidi watakaoweza kupatikana.
Na endapo itadhihirika kwamba tuhuma
zina uzito, mtuhumiwa atatitwa mbele ya kikao cah Kamati ya Usalama na Maadili
ya ngazi inayohusika, kama ni lazima, ili apate kuhojiwa ana kwa na.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa
Madam Jesca Msambatavangu
No comments:
Post a Comment