Tuesday 4 August 2015
MAGUFULI URAISI CCM ACHUKUA FOMU
MGOMBEA kiti cha Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi, CCM, John Pombe
Magufuli, leo Jumanne Agosti 4, 2015, amechukua fomu za uteuzi za Tume
ya Taifa ya Uchaguzi, NEC, tayari kwa mchakato wa kutafuta wadhamini 200
ambao ni raia wa Tanzania wenye shahada za kupigia kura. Magufuli
ambaye alifuatana nna mgombea mwenza wake, Samia Suluhu Hassan, Katibu
Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana, na viongozi na wafuasi wa CCM,
alkiambiwa na maafisa wa tume hiyo nkuwa, sasa yampasa kuzunguka mikoa
10 ya Tanzania ikiwemo walau miwili ya Zanzibar, ili kupata wadhamini
hao na akimaliza zoezi hilo atapaswa kurejesha fomu hizo kabla ya Agosti
20, 2015.Pichani Maghufuli na mgombea mwenza wake, wakiwa kwenye gari
la wazi, wakipungia mkono wananchi huku mkoba wenye fomu hizo ukiwa
mbele yao. Maelfu ya wafuasi wa chama hicho, walijaa mabarabarani
kuanzia barabra ya Ohio, Bibi Titi Mohammed na ile ya Lumumba, na
kusababisha shughuli za kawaida kwenye maeneo hayo kusimama kwa muda ili
kupisha shamrashamra hizo. Baada ya msafara ya Magufuli kutoka tume ya
taifa ya uchaguzi, ulipokelewa na mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya
Kikwete kwenye opfisi ndogo za makao makuu hya CCM, Lumumba jijini Dar
es Salaam, ambapo Magufuli aliwaonyesa wafuasi wa CCM fomu hizo na
kuwaambia sasa kazi imeanza. Magufuli anatarajiwa kupambana na mgombea
wa vuguvugu la Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, Waziri mkuu wa zamani
Edward Lowassa, ambaye alikihama chama hicho na kujiunga na chama kikuu
cha upinzani CHADEMA, ambacho tayari kimemtangaza kuwa mgombea wake na
kwa hali hiyo ndiye atakuwa mgombea wa UKAWA kutokana na makubakiano ya
vyama vinavyounda umoja huo ambavyo ni CUF, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na
NLD. Uchaguzi mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment