MWENYEKITI
wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha, Elias Ngorisa,
(Katikati, akizungumza kwa niaba ya madiwani 18 wa kutoka CCM, wilayani humo,
wambao wamejivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na CHADEMA Agosti 5,
2015. Madiwani hao walipokelewa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh. Joshua
Nasari, (wapili kushoto).
NA K-VIS MEDIA
NA K-VIS MEDIA
WIMBI la
wanachama wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, kukihama chama hicho linazidi kukua,
ambapo Agosti 5, 2015, madiwani 18 wa Halmashauri ya Wilaya ya
Ngorongoro, akiwemo mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Elias Ngorisa
wamejivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na CHADEMA.
Akiwawakilisha
madiwani hao waliohama, Ngorisa aliyeambatana na Katibu wa fedha na uchumi wa
CCM wilayani humo, Kagil Ngukwo, ambaye alikuwa diwani wa Kata ya Engusero
Sambu, walikabidhiwa kadi mpya wa CHADEMA na Mbunge wa Arumeru Mashariki,
Joshua Nasari maarufu kama “Dogo Janga”.
Pia wazee
wa kimila wa Kabila la Kimasai (malaigwanani) Lekakui Oleiti na Laurence
Ngorisa, wote kutoka Engusero Sambu, walihudhuria tukio hilo la kujiunga na
CHADEMA.
Akizungumza
wakati wa tukio hilo la kupokea kadi za CHADEMA, Ngorisa, alisema wapo
madiwani 18 kati ya 28 ambao tayari wamechukua kadi za Chadema.
“Leo
(jana) tumewawakilisha hapa, lakini wamekwishakihama Chama Cha
Mapinduzi…madiwani hao watatetea nafasi zao katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25,
mwaka huu.
“Nimeshawishika
kwa dhati kabisa kubadili mwelekeo wa awali na kuwa mwanachama wa Chadema.
“Sisi
tumehamia CHADEMA kwa vile tunataka mabadiliko na mjuelekeo ulivyo mabadiliko
yako huku CHADEMA na sio CCM.” Alisema Ngorisa.
“Kilichotusukuma
kuhamia CHADEMA, ni kumuunga mkono mgombea wa kiti cha Rais wa Tanzania kupitia
UKAWA Mh. Edward Lowassa.”
Tangu
atangaze kukihama chama cha Mapinduzi mwishoni mwa mwezi uliopita, Mh. Edward
Lowassa, alisema, uamuzi aliouchukua ni mgumu kwa vile nia yake ya kuwaondolea
umasikini Watanzania bado iko palepale, na kwa vile anatambua Watanzania
wanataka mabadiliko, basi mabadiliko hayo yatapatikana nje ya CCM.Tayari
madiwani wengine kadhaa wa wilaya ya Monduli, wamekwisha ihama CCM muda mfupi
baada ya mkutano mkuu wa CCM uliomalizika mwezi uliopita mkoani Dodoma,
wakisema kuwa hawakuridhishwa na mchakato wa kumpata mgombea wa kiti cha Rais
wa Tanzania kupitia chama hicho, ambapo, aliyekuwa Mbunge wa Monduli na Waziri
Mkuu wa zamani Mh. Edward Lowassa, alikatwa jina lake katika hatua za awali za
vikao vya chama hicho
No comments:
Post a Comment