Thursday 20 February 2014

ELIMU YA STADI ZA MAISHA YATOLEWA MUFINDI KASKAZINI.




MUFINDI
Shirika lisilo la kiserikali laMufindi youth and women for rulal development (MUYOWIRUDE) kwa kushirikiana na Mgimwa Foundation  limejipanga kutoa  elimu ya ujasiliamali kwa vijana katika mashindano ya ligi ya maendeleo vijijini yanayoendelea katika kijiji cha Vikula kata ya Ihalimba ili kuondokana na adha ya ajira vijijini.
Akizungumza Mkurugenzi wa  shirika Muyowirude Marco Shayo alisema kuwa michezo hii imewakutanisha vijana wa vijiji na kata mbalimbali hivyo ni bora kuwasaidia kwa kuwapa elimu ya ujasiliamali pamoja na kuwashauri vijana juu ua upimaji afya zao.
Shayo alibanisha kuwa vijana hao wanajifunza jinsi ya kutengeneza sabuni , batiki na nguo pamoja na kuwashauri kujiunga katika vikundi vya pamoja na ili kuweza kupata mkopokwa urahisi.
“Tunatoa elimu hii kwa vijana ili waweze kujishughulisha na sio kukaa bila kazi na hatimaye kukimbilia mjini ambapo wataenda kupata tabu na kuishia kuwa vibaka au watoto wa mitaani”alisema Shayo

Kwa upande wao vijana hao walisema kuwa wanalishukuru sana shirika hilo kwa kuwapatia elimu hiyo kwani wamejifunza mengi na hawaoni sababu ya kukimbilia mjini kutokana na kwamba hata vijijini wakiwezeshwa wanaweza kufanikiwa katika maisha.
“Tumekuwa tukikimbilia mjini kwa sababu wanasema mjini ndio mambo yote lakini tumegundua kwamba hata vijijini pia mtu unaweza ukafanya biashara zako na kuepuka kukimbilia mjini bila kazi ya kufanya”alisema Anania
Berdina  & Mnyalu.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment