Thursday 20 February 2014

MGIMWA FOUNDATION MUFINDI YA ZINDUA MICHEZO





MUFINDI
TIMU  ya mpira wa miguu Vikula Fc imeibuka ushindi wa bao mbili kwa moja  dhidi ya timu ya Nundwe Fc ambapo mashindano hayo yalifanyika katika kijiji  cha Vikula cha kata ya Ihalimba wilayani  ya Mufindi.
Timu ya Vikula ilijipatia goli la kwanza kunako  dakika ya 15 kupitia mchezaji wake mahili Runy Mkiwa .
Goli la pili lilifungwa na Anania mwagama dakika ya 43 huku Muhiche  akiifungia timu ya Nundwe  Fc bao moja kunako dakika ya 65.
Akizindua mashindano hayo ya ligi ya maendeleo vijijini kata ya Ihalimba mkurugenzi wa Halimashauri ya Mufindi Peter Tweve alisema kuwa michezo ni sehemu ya kuleta umoja na amani kwa vijana hivyo halimashauri itaendelea kusaidiana na shirika la Muyowirude pamoja na mgimwa foundation kuhimiza michezo vijijini kama njia ya kujifunza .
Tweve alizikabidhi timu zitakazo shiriki mashindano hayo Jezi na mipira yenye thamani ya Tsh.1milioni timuhizo ni Nundwe, Ihalimba, Usega, Vikula, Wamimbalwe na Ufungu secondary.
Zawadi zingine zitakazotolewa ni pamoja zawadi  kwa mshindi wa kwanza jezi na mipira yenye thamani ya shilingi laki tano,
Mshindi wa pili atazawadiwa jezi na mpira wenye thamani ya shilling laki tatu,na mshindi wa tatu atapewa shilling laki moja na elfu hamsini.
Mchezaji mwenye nidhamu atazawadiwa kiasi cha shilling elfu hamsini zawadi hizo zinathamani ya shiliing million.
Fainali ya mashindano hayo yatafanyika march 13 mwaka huu katika kijiji cha Vikula kaya ya Ihalimba wilaya ya Mufindi.
MWISHO.
Mnyalu&Berdina
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment