Thursday 13 February 2014

KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI YAANZA KUSIKILIZWA


Na: BerdinaMajinge,Iringa

MAHAKAMA kuu kanda ya Iringa imeanza kusikiliza kesi ya muuaji wa aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha channel ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi huku vituko na visa baina ya wanahabari na askari wa jeshi la polisi mkoani Iringa vikiendelea kuchukua sura mpya hali inaleta maswali miongoni mwa wafuatiliaji wa kesi hiyo.
katika kesi hiyo wakili wa serikali Adolph Maganda amedai mahakamani hapo mbele ya Jaji Mary Shangali kuwa mnamo tarehe 2 septemba mwaka 2012 askari no g. 2573 wa jeshi la polisi kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Iringa Pasificus Ceophace simon alimuua Daudi Mwangosi kwakukusudia kinyume na kifungu cha kanuni ya adhabu no 196 sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002
Wakili huyo wa serikali amewasilisha mahakamani hapo vielelezo vya ushahidi wa kesi hiyo ikiwemo ripoti ya kitabibu iliyotolewa na mganga aliyefanyia uchunguzi mwili wa marehemu mwangosi, kitabu cha kumbukumbu za kutoa na kurudisha silaha kituoni, ripoti ya mtaalam wa milipuko, mahojiano ya ungamo na onyo pamoja na gazeti la mwananchi la tarehe 3 septemba 2012 lenye picha ya mtuhumiwa akiwa ameshikilia silaha aliyoitumia kumfyatulia marehemu
Hata hivyo mtuhumiwa licha ya kukiri kuwepo katika eneo la nyololo wilayani mufindi siku hiyo ya tukio amekana shitaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa mpaka hapo itakapopangiwa siku ya kusikilizwa tena na mtuhumiwa amerudishwa rumande
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mwandishi wa habari wa magazeti ya Dairy News na Habari leo mkoani iringa Frank Leonard alikamatwa na polisi kwa tuhuma za kupiga picha wakati mahakama ikiendelea ambapo alishikiliwa kwamuda na baadae kufikishwa katika kituo cha polisi iringa kabla ya kuachiwa bila kuandika maelezo.
mwisho

Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment