Saturday 22 February 2014

WAZIRI ASITISHA UJENZI WA STEND YA IGUMBILO


 Dk Mahenge akiwa na viongozi wa mkoa na Manispaa ya Iringa katika eneo linalolalamikiwa na wadau wa maji, lisijengwe stendi hiyo
Wakiangali Mto Ruaha Mdogo



IRINGA.
SERIKALI imeagiza  Baraza la Taifa la Mazingira NEMC kufanya upya tathmini ya athali ya kimazingira katika eneo linalotarajiwa kujengwa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani katika manispaa ya Iringa huku pia kiitaka Manispaa hiyo kusimamisha uendelezwaji wa eneo hilo kusubiri tathimini hiyo.
Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa Rais anayeshughulikia mazingira Dokta Binilith Mahenge ametoa agizo hilo mjini Iringa mara baada ya kutembelea na kukagua eneo hilo la Igumbilo lililotengwa na Manispaa ya Iringa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha mabasi na kuzusha mgogoro na wadau mbalimbali wa mazingira.
Awali mkuu wa mkoa wa Iringa Dk Christine Ishengoma , alimweleza Waziri huyo kuwa kutokana na kukua kwa haraka na ongezeko la watu katika mkoa wa Iringa manispaa inahitaji kuwa na kituo cha mabasi cha kisasa ili kutoa huduma inayostahili kwa wasafiri .
Aidha aliongeza kuwa  kutokana na uwepo wa chanzo cha maji katika eneo hilo ni vema kufanya tathimini yakutosha ya athali za kimazingira ili mradi huo usiathili mazingira na huduma nyingine.
kwa upande wake afisa wa maji bonde la rufiji Idris Msuya alisema jiografia ya eneo hilo ni tata kutokana na sheria ya mazingira kutokuwa wazi katika baadhi ya maeneo kwani eneo chepechepe katika eneo hilo la Igumbilo limeendelea hadi nje ya mita zinazotajwa na sheria ya mazingira hivyo ni vema kufanya tathimini inayotazama athali zote za kimazingira katika eneo hilo.
Ujenzi wa kituo hicho cha mabasi cha Igumbilo katika manispaa ya Iringa umezua mgogoro baina ya mamlaka mbalimbali ikiwemo mamlaka ya maji na usafi wa mazingira mjini Iringa IRUWASA, bonde la maji la Rufiji na wadau wa mazingira kwa upande mmoja na manispaa ya Iringa iliyopitisha ujenzi wa kituo hicho zaidi ya miaka sita iliyopita
MWISHO.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment