VIONGOZI MBALIMBALI WAKIKAGUA MASHAMBA KATIKA KIJIJI CHA KANING'OMBE WILAYA YA IRINGA VIJJINI.
KANING’OMBE,
IRINGA
PAMOJA na
uwepo wa ardhi ya kutosha na yenye rutuba kwa ajili ya kilimo nchi nyngi barani
afrika zimeshindwa kufikia azimio la maputo la mwaka 2003 ambapo wakuu wa nchi
za afrika walikubaliana kila nchi kutenga kiasi cha asilimia kumi ya bajeti ya
kitaifa kwaajili ya maendeleo ya sekta ya kilimo
Hayo yalisemwa
katika kongamano la kuzindua mwaka wa kilimo afrika lililofanyika katika kijiji
cha Kaning’ombe mkoani Iringa ambapo mgeni rasimi makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Manzania Dokta Mohamed Gharib bilali aliwakishwa na mkuu wa mkoa wa
Iringa Dokta Christine Ishengoma.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la ANSAF
Audax Rukonge walioandaa kongamano hilo alisema hadi sasa ni Nchi nane tu ndiyo
zimeweza kufikia makubaliano hayo ya Maputo.
Rukonge alisema
kuwa azimio hilo lilikubaliwa na viongozi hao na kuona
kuwa kinatosha kuchangia pato la pato la taifa na kuongeza uzalishaji
na kukuza sekta ya kilimo hapa nchini kwa asilimia sita ambapo
litawasaidia kuodokana na umasikini hapa nchini.
kuwa kinatosha kuchangia pato la pato la taifa na kuongeza uzalishaji
na kukuza sekta ya kilimo hapa nchini kwa asilimia sita ambapo
litawasaidia kuodokana na umasikini hapa nchini.
Akizungumza
kwa niaba ya makamu wa rais mkuu wa mkoa wa Iringa DK Christine Ishengoma alisema
tatizo la pembejeo bado ni kubwa kwa wananchi wa kipato cha chini hasa maeneo
ya vijijini hivyo ni vema serikali ikaangalia uwezekano wa kuagiza mitambo ya
kilimo kama matrekta mapya na yaliyotumika ili kuwezesha wakulima kumudu
kuyanunua.
kwa
upande wake katibu tawala wa mkoa wa Iringa bibi Wamoja Ayubu alisema kutokana
na changamoto ya pembejeo za kilimo na mitaji mkoa wa Iringa wenye eneo la
zaidi ya hekta 54 elfu zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji umeweza kutumia
kiasi cha hekta 25 elfu sawa na asilimia 47 ya eneo lote.
Mmoja wa
wakulima wa kijiji cha Kaning’ombe bwana Ausebio Mbangile akieleza athali za
kukosekana kwa trekta la kulimia kijijini hapo alisema kuwa katika kilimo kimekuwa
ni changamoto kubwa kutokana na
kukosekana kwa masoko, kukodisha matekta kwa bei kubwa, miundombinu pamoja na pembejeo kuwa bei kubwa na kushindwa kuzimudu.
Mbangile alisema kuwa pamoja na changamoto hiyo amekuwa akiuza gunia
lenye ujazo wa kilo 150 kwa shilingi 380,000 na kupata hasara kubwa
na hivyo kumrudisha nyuma kimaendeleo.
kukosekana kwa masoko, kukodisha matekta kwa bei kubwa, miundombinu pamoja na pembejeo kuwa bei kubwa na kushindwa kuzimudu.
Mbangile alisema kuwa pamoja na changamoto hiyo amekuwa akiuza gunia
lenye ujazo wa kilo 150 kwa shilingi 380,000 na kupata hasara kubwa
na hivyo kumrudisha nyuma kimaendeleo.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment