Monday 27 January 2014

FAINALI YA MGIMWA CUP MUFINDI KASKAZINI.


Wachezaji wa timu ya Ugenza na Ukeremi   wakiwania mpira wakati timu zao zilipo pambana katika fainali ya mashindano ya Mgimwa cup.Mchezo huo ulichezwa katika kiwanja cha shule ya msingi Ikweha na timu ya Ugenza kuibuka washindi wa magoli mawili dhidi ya Ukeremi ambao hawakupata kitu
Hivyo Ugenza wameibuka washindi wa mashindano hayo na Ukeremi kuibuka nafasi ya Pili huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na timu ya Sinai.
 Afisa mtendaji  wa kata ya Ikweha  Mathiasi  Mkakanzi akiongea na wanaanchi wakati wa kilele cha mashindano ya Mgimwa cup Mufindi kaskazini.
 Wananchi wakata ya Ikweha na vitongoji vyake walio hudhuria uwanjani kuiona fainali ya michuano ya Mpira wa miguu Mgimwa Cup Mufindi kaskazini. jana.
 Wananchi waliojitokeza kupata ushauri nasaha na upimaji wa vvu kwa hiyari wakiwa katika msitali ili kupata huduma hiyo.
Jumla ya wliopima 75 wanawake 45 wanaume 30 walioathilika 4 wanawake 1 wanaume3.
Baadhi ya viongozi wa Serikali Mufindi wakiangali mpira wamiguu
wakati wa fainali ya Mgimwa Cup.kata ya Ikweha

                            Hakuna kupita hapa pambano linaendelea.


 Wapenzi na mashabiki wa mpira wa miguu wa kiangalia fainali ya Mgimwa Cup.
 Mh Evarist kalalu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mufindi kulia kwake akifuatilia mpambano huo.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment