Monday 27 January 2014

ZAWADI KWA WASHINDI MGIMWA CUP MUFINDI


 Mh.Bi Evarista kalalu mkuu wa wilaya mufindi. akikabidhi Jezi set mbili na Mpira kwa Zamoyoni kifumbe  na hodha watimu ya Ugenza zenye thamani ya Tshs,500000/=Kwakuibuka washindi katika mashindano ya Mpira wa miguu Mgimwa Cup kata ya ikweha
 Nahodha Willy Mkulu wa timu ya Ukeremi akipokea Zawadi ya ushindi wa pili kwa mashindano zenye thamani ya Tsh.350,000/=
 Msanii wa muziki wa Bongo flevar akitumbuiza kwenye hafla ya kuwazadia washindi wa mashindano ya Mgimwa Cup
 Mkuu wa wilaya Mufindi Bi Evarista kalalu akiongena wananchi wa kata ya Ikweha mufindi kaskazini
 Nahodha wa timu ya Sinai akipokea zawadi ya mipira miwili kwa Mkuu wa wilaya Mufindi  ikiwa ni zawadi ya Mshindi wa tatu katika yenye thamani ya Tshs 50000/=.



 Picha zote na Mnyalu

MUFINDI.
WANANCHI wa kijiji cha Ikweha wamewaomba baadhi ya viongozi kutokuwa na mtazamo hasi kwa viongozi kwa kupandikiza chuki na kuwanyima fursa vijana kutokana na ikitadi zao za kisiasa.
Hayo yalisemwa na Kabula Kidai wakati akisoma risala wakati wa fainali za mashindano ya Mgimwa cup  sambamba na elimu ya stadi za maisha kwa Vijana vijijini chini ya ushirikiano wa Mufindi youth and women for rulal development(MUYOWIRUDE ) na Mgimwa Foundation yaliyofanyika katika kata ya Ikweha  kijiji cha Ikweha wilayani Mufindi kaskazini.
Kabula alibainisha kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakipandikiza chuki kwa vijana na kuwanyima fursa zinazojitokeza pamoja na kuwapa elimu ya ujasiliamali kwa manufaa yao binafsi.
Kwa upande wake mgeni rasimi mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarsta Kalalu alisema kuwa elimu ya ujasiliamali itaepusha adha ya vijana wengi kukimbilia mjini hivyo wajishughulishe na michezo na kuondokana na makundi yasiyofaa na kukaa vijiweni.
“vijana wajiunge katika vikundi ili muweze kupata msaada wa kimaendeleo kama mikopo,elimu ya ujasiliamali pamoja shughuli za kimaendeleo.
Sambamba na michezo wahudumu wa Afya ya msingi walitoa elimu ya ushauri nasaha na upimaji wa virusi vya ukimwi.
Jumla ya wananchi waliojitokeza kupima sabini na tano wanawake arobaini na tano  na wanaume thelasini  kati ya hao walio patikana na maambukizi ni wanne  mwanamke mmoja na wanaume watatu.
Said Ng’amilo.
MWISHO.



MUFINDI.

TIMU ya mpira wa miguu ya Ugenza imeibuka ushindi wa bao 2 kwa nunge dhidi ya timu ya Ukeremi katika fainali ya kombe la Mgimwa cup lililomalizika jana katika kijiji cha Ikweha kata ya Ikweha wilayani Mufindi.
Goli la kwanza lilifungwa na mshambuliaji mahili kutoka timu hiyo Oscar mdema kunako dakika ya 35 katika kipindi cha kwanza ambapo mshambuliaji huyo alipata pasi kutoka kwa kiungo mwenye jezi 12 mgongoni Zamoyoni nyange na kupachika goli hilo.
Frenki kapende aliifungia timu hiyo gori la pili kunako dakika ya 83 katika kipindi cha pili na kusababisha mashabiki wa timu hiyo kuwanyenyua jukwaani na kushangilia ushindi kwa furaha huku timu ya Ukeremi kunyong’onyea kwa kupachikwa mabao hayo.
Mpaka kufikia mwisho wa mchezo timu ya Ugenza iliibuka ushindi na kujinyakulia zawadi ya seti ya jezi za traki suti 16 na mipira miwili yenye thamani ya shilling laki tano,ikifatiwa na timu ya Ukeremi ambapo ilipata full jezi na mpira mmoja zenye thamani ya shilling laki tatu na elfu hamsini..
Mshindi wa tatu ambaye ni timu ya Sinai ilipata mipira miwili yenye thamani ya shilling laki moja na elfu hamsini,
Timu zilizoshiriki mashindano hayo tangu mwanzo wa fainali hiyo zilikuwa sita ambazo ni Ugenza,Ukeremi,Uyela,Ikweha,Sinai,Ilangamoto na hatimae kufika mwisho wa fainali zikiwa zimebaki timu nne ambapo timu ya Ikweha na Ilangamoto kujitoa michezoni.
Michezo hiyo ambao ulizaminiwa na Mgimwa Foundation chini ya ushirikiano wa  Mufindi youth and women for rulal development(MUYOWIRUDE)  Kwa lengo la kuleta maendeleo vijijini kwa vijana na kuwaepushia adha ya vijana wengi kukimbilia mjini ili hitimishwa .
MWISHO.















Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment