Iringa. zaidi ya kaya 23 ikiwemo shule ya msingi izazi zimeezuliwa na upepo kufuatia mvua iliyonyesha katika kijiji cha Izazi wilayani Iringa ikiambatana na upepo mkali na kusababisha wakazi hao kukosa mahari pa kuishi.
wamekabidhi msaada wa zaidi ya tani
tano za chakula ikiwemo kilo mia tisa za maharage na lita sitini za mafuta ya
kupikia kwa wahanga Benki ya NMB tawi la mkwawa mjini Iringa walisema kuwa
wahanga hao walioezuliwa nyumba zao tarehe 12 mwezi huu kufuatia na mvua
iliyonyesha pamoja na upepo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi
msaada huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni tano meneja wa NMB tawi
la Iringa Sumka Mbuba alisema msaada huo umetokana na benki hiyo kuguswa na
kadhia waliyoipata wananchi wa kijiji cha Izazi hasa ikizingatiwa kuwa wakati
huu ni wa kilimo ambapo wananchi hao wanatakiwa kuwa katika kazi za uzalishaji
hivyo wameona haja ya kuwasaidia kuwapunguzia mzigo wa adha hiyo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa
halmashauri ya Iringa Steven Muhapa aliishukuru benki hiyo kwa kuitikia haraka
ombi la halmashauri kuwaomba wadau mbalimbali kusaidia wananchi hao ili
kuwafanya warudie katika hali yao ya awali .
Kwenyekiti wa kamati ya maafa
Leonard Msigwa alisema kuwa hasara iliyotokana na maafa hayo ni zaidi ya
shilingi milioni 30.
Mwananchi ilishuhudia baadhi ya
wananchi wakiendelea na ukarabati wa kurudishia mapaa katika nyumba zao huku
pia mafundi wakiwa kwenye harakati za kurudishia paa katika madarasa
yaliyoezuliwa katika shule ya msingi izazi huku masomo yakiwa yanaendelea
shuleni hapo ambapo walimu wamelazimika kutumia vivuli vya miti kama ofisi za
muda baada ya ofisi yao kukumbwa na dhahma hiyo
Mnyalu.
Moja ya nyumba ilio ezuliwa
No comments:
Post a Comment