Tuesday 28 January 2014

MICHEZO NA STADI ZA MAISHA KWA VIJANA MUFINDI




MUFINDI KASKAZINI.
WANANCHI wa kijiji cha Ikweha wamewaomba baadhi ya viongozi kutokuwa na mtazamo hasi kwa viongozi kwa kupandikiza chuki na kuwanyima fursa vijana kutokana na ikitadi zao za kisiasa.
Hayo yalisemwa na Kabula Kidai wakati akisoma risala wakati wa fainali za mashindano ya Mgimwa cup  sambamba na elimu ya stadi za maisha kwa Vijana vijijini chini ya ushirikiano wa Mufindi youth and women for rulal development(MUYOWIRUDE ) na Mgimwa Foundation yaliyofanyika katika kata ya Ikweha  kijiji cha Ikweha wilayani Mufindi kaskazini.
Kabula alibainisha kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakipandikiza chuki kwa vijana na kuwanyima fursa zinazojitokeza pamoja na kuwapa elimu ya ujasiliamali kwa manufaa yao binafsi.
Kwa upande wake mgeni rasimi mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarsta Kalalu alisema kuwa elimu ya ujasiliamali itaepusha adha ya vijana wengi kukimbilia mjini hivyo wajishughulishe na michezo na kuondokana na makundi yasiyofaa na kukaa vijiweni.
“vijana wajiunge katika vikundi ili muweze kupata msaada wa kimaendeleo kama mikopo,elimu ya ujasiliamali pamoja shughuli za kimaendeleo.
Sambamba na michezo wahudumu wa Afya ya msingi walitoa elimu ya ushauri nasaha na upimaji wa virusi vya ukimwi.
Jumla ya wananchi waliojitokeza kupima sabini na tano wanawake arobaini na tano  na wanaume thelasini  kati ya hao walio patikana na maambukizi ni wanne  mwanamke mmoja na wanaume watatu.
Said Ng’amilo.
MWISHO.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment