Thursday 8 May 2014

MAREHEMU GERVAS KALOLO KUZIKWA LEO IRINGA MJINI.




1.                WASIFU WA MAREHEMU   KUZALIWA
Marehemu GERVAS  JOHN KALOLO alizaliwa tarehe 09.11.1964 katika Hospitali ya mkoa wa Iringa

2.      ELIMU
Marehemu GERVAS  JOHN KALOLO  alisoma shule ya awali na msingi katika shule ya msingi CHEM CHEM  hapa iringa mjini na kuhitimu mwaka 1980 na baadae aliendelea na masomo ya Sekondari katika shule ya Sekondari HIGHLANDS  na kuhitimu kidato cha nne mwaka 1983.

3.      AJIRA
Mnamo mwaka 1985 marehemu aliajiriwa katika kampuni ya IMAC ambako alifanya kazi kwa muda mfupi. Na baadae aliacha kazi  na kuamua kujishughulisha na shughuli binafsi za Ujasiriamali na pia aliingia rasmi katika shughuli za kisiasa.

4.      UONGOZI KATIKA SIASA
Baada ya kuingia katika siasa mnamo mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwenyekiti  wa mtaa.Na ilipofika mwaka 2005 alichaguliwa kuwa Mheshimiwa Diwani kupitia tiketi ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM) mpaka mwaka 2010. Mwaka huo huo 2010 aliamua kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na mpaka umauti unamkuta  alikuwa  mmoja wa viongozi wa CHADEMA hapa Iringa.
5.      UONGOZI KATIKA KANISA
Marehemu GERVAS KALOLO alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Miyomboni Parokia ya Consolata – Mshindo.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment