Friday 2 May 2014

MBUNGE JIMBO LA KALENGA AANZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO.




MBUNGE JIMBO LA KALENGA AANZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO.  
Mh Godfray Mgimwa mbunge wa Jimbo la Kalenga  amefanya ziara ya kuwashukuru wananchi  katika baadhi ya kata Jimboni humo pamoja na kutoa vifaa vya ujenzi vilivyo ahidiwa na Mh marehemu Wiliam Mgimwa  sambamba na yeye binafsi  kutoa sehemu ya vifaa na kuahidi kuchangia zaidi na kutatua changamoto Sawa na mahitaji sehemu husika.

Akiongea na wananchi wa kijiji cha Tanangozi ,Kiwere, Itagutwa ,ibumila katenge na Mgama vilivyopo  Wilaya ya Iringa  Mh Godfray  Mgimwa alisema ameamua kufanya ziara mapema baada ya Kuchaguliwa ilikutoa shukurani kwa wananchi waliomchagua katika uchaguzi uliofanyika 16/03/2014.

Mh Mgimwa alisema pamoja na kuwa zipo changamoto nyingi katika maendeleo ataanza na baadhi sawa na umuhimuwake kwa nafasi yake yale ambayo yanapaswa kufanywa na ngazi za juu atawasilisha kwa wahusika kama Raisi na Mawaziri.

sambamba na hilo Mh Godfray Mgimwa ametoa ahadi ya bati 100 kwa ajili ya Shule ya Sekondari Tanangozi ambayo wanakijiji wameanza harakati za ujenzi Wakiwa wameisha andaa Tofari,Mawe na Mchanga ili kufanikisha ujenzihuo juhudi zaidi zinahitajika toka kwa wana kijiji kwakuzingatia kunampango wa kata ya Mseke kuwa kata mbili Mseke A na B.

Mh Mgimwa alisema amepokea kwa heshima kubwa kuchaguliwa kwake pamoja na yote yaliojiri katika harakati za uchaguzi binafsi yeye atakuwa pamoja na wananchi wa Kalenga kwahali na mali wakati wowote akiongea na wananchi katika mkutano uliofanyika ndani ya Ofisi ya Kijiji cha Tanangozi. 

Awali Mh Mgimwa amefanya kikao na Waheshimiwa  Madiwani  wa jimbo zima la Kalenga na kubadilishana nao mawazo juu ya maendeleo ya Kalenga na Changamoto zilizopo katika kila kata pamoja na kuangalia uwezekano wa kuondoa makundi ndani ya CCM Jimbo la Kalenga ilikuwe na Mshikamano wa dhati kwamaendeleo ya Chama na Wananchi kwajumla.

 Ziara yake hiyo ilianzia katika Tarafa ya Kalenga kata ya Kiwere  na kutoa Bati themanini zenye thamani ya Tsh,1,400,000/= kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiwere na pia amekabidhi bati Hamsini zenye thamani ya Tsh.875,000/= katika shule ya msingi  Itagutwa.

Kwa upandewake  Mgimwa amekabidhi bati hamsini kwa ajili ya Ujenzi Shule ya Msingi Makota  pamoja na kuahidi kuitembele Shule ya Msingi Ugwachanya ambayo haina nyumba za waalimu na Madarasa yapo katika hali mbaya ilikuona namna atakavyo shiriki .

SHULE ya Msingi Ibumila iliyopo katika kata ya Mgama Tarafa ya Mlolo  inakabiliwa na ukosefu wa choo  cha  shule na kusababisha shule hiyo ufungwakwa muda.

Akisoma taarifa ya kijiji mbele ya Mbunge wa jimbo la kalenga Godfrey Mgimwa  Diwani wa kata ya Mgama Denisi Lupala alisema kuwa shule hiyo ilifungwa kwa muda kutokana na choo hicho kutumbukia na kusababisha shule kukosa choo kabisa ingawa sasa wanafunzi wanatumia choo cha muda wakati ujenzi unaendelea.

“licha ya shule ya msingi Ibumila kufungwa kutokana na choo kutumbukia pia Kijiji hakijawahi kuwa na Zahanati  vilevile kuna tatizo la Barabara inayo unganisha kijiji hicho na kijiji cha Ilandutwa kuelekea Mufindi”alisema Lupala

Lupala aliongeza kuwa kijiji hicho kimekuwa katika ujenzi wa nyumba ya mwalimu wa shule ya msingi  Mgama kwa muda wa miaka saba sasa ikiwa na ukosefu wa milango na madirisa hivyo wanaitaji msaada ili kufanikisha ujenzi huo.

Kwa upandewake Mh Mgimwa alitoa  simenti mifuko 30 yenye thamani ya Tsh435,000/= kwa ajili ya ujenzi wa choo na zahanati huku akiahidi kuchangia kiasi cha Tsh.milioni mbili kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.

pia alitoa Bati miamoja  zenye thamani ya Tsh milioni moja  laki saba na hamsini  kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Waalimu Sekondari ya Mgama  

Mbunge a jimbo la Kalenga Mh Godfery Mgimwa ametoa bati 50 na mipira mitano yenye thamani ya shilingi million moja na laki moja   katika isupilo kata ya Lumuli kwa ajili ya zahanati ya kijiji hicho.
Awali akisoma taarifa ya kijiji hicho Edward Mbwilo mtendaji wa kijiji cha Isupilo alisema kuwa kijiji hicho kinakabiliwa na ukosefu wa zahanati ya kijiji ambapo ndio wapo katika harakati za ujenzi wa zahanati hiyo pamoja na shule ya msingi..

Mbwilo alisema kuwa wanashukuru kwa msaada huo ambao utawezesha kufanikisha zoezi la ujenzi huo pamoja na shule.
Kwa upande wake Mgimwa alisema kuwa kama mbunge atafanya kazi kwa watu wote wa vyama vyote bila kubagua ili kupata maendeleo .

“mimi nachangia mabati 50 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati na mipira 5 kwa ajili ya vijana wa kijijini hapa ili kujishughulisha na michzo hivyo basi naomba tufanye kazi kwa pamoja”alisema Mgimwa.

Aidha katka kijiji cha Muwimbi kilichopo kata ya Lumuli tarafa ya kiponzelo Mgimwa alitoa mabati 80 yenye thamani ya shilingi mil 1 na laki 4 kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule ya sekondali ya Lumuli.

Diwani wa kata hiyo alisema kuwa wanakabiliwa na ukosefu wa bati kwa ajili ya kuezeka bweli hilo ambalo tayari kijiji kimejenga na kufikia hatua hiyo.

Aidha kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme pamoja na daraja ambalo wanafunzi  wanatakiwa kuvuka kwa kipindi cha mvua wanafunzi wengi hushindwa kufika shule.
Mbunge huyo wa kalenga ameahidi kiasi cha shilingi million 1 kwa ajili ya vikundi sita vya vikoba vilivyopo kijijini hapo.

Katika kijiji cha Mibikimitali  kata ya Ifunda  alikabidhi bati 50 kwa ajili ya ujenzi wanyumba  ya mwalimu katika shule ya msingi mibiki mitali kutokana ukosefu wa nyumba ya walimu katika kijiji hicho.

Aidha akisoma taarifa ya kijiji hicho Gervas Ndendya kwa niaba ya afisa mtendaji alisema kuwa kijiji hicho kinakabiliwa na ukosefu wa chumba cha kupumzikia wagonjwa katika zahanati ya kijiji hicho.

Ndendya alisema kuwa kijiji hicho pia kinakabiliwa na ukosefu wa maji katika zahanati pamoja na matumizi kwa wanakijiji kwa sababu kijiji hicho hakina kisima cha maji wala bomba.

Ukosefu wa umeme hivyo hulazimika kufanya kazi hasa usiku kwa kutumia tochi hata katika huduma ya uzalishaji hivyo wanaomba kila nyumba ifungiwe sola yake ili kurahisisha upatikanaji wa umeme katika zahanati.
Mnyalu.
Unknown Web Developer

No comments:

Post a Comment